1. Wimbi la maisha likutosapo, Unakata tamaa ushindwapo, Hesabu baraka, kwa mojamoja, Wema wa Mungu utakushangaza.
Zihesabu; Kwa mojamoja. Zihesabu; Ona ya Bwana. Zihesabu; Kwa mojamoja. Hesabu baraka; Ona ya Bwana.
2. Je, unaelemewa na mzigo? Msalaba wakushinda uzito? Hesabu baraka; shaka ziishe, Na kisha utaimba siku zote.
Zihesabu; Kwa mojamoja. Zihesabu; Ona ya Bwana. Zihesabu; Kwa mojamoja. Hesabu baraka; Ona ya Bwana.
3. Uwaonapo wengine na mali, Kumbuka ahadi zake Mwokozi. Hesabu baraka; wingi wa pesa Haununui ufalme wa Bwana.
Zihesabu; Kwa mojamoja. Zihesabu; Ona ya Bwana. Zihesabu; Kwa mojamoja. Hesabu baraka; Ona ya Bwana.
4. Hivyo matatizo yakukumbapo, Mungu yupo nawe, usife moyo. Hesabu baraka; na utajaliwa Malaika watakusaidia.
Zihesabu; Kwa mojamoja. Zihesabu; Ona ya Bwana. Zihesabu; Kwa mojamoja. Hesabu baraka; Ona ya Bwana.