Book cover

Huenda Isiwe Juu Ya Kilele Cha Mlima

Nyimbo Za Dini Pamoja Na Nyimbo Za Watot, 44


1. Labda siyo kwenye milima Wala penye tufani, Labda siyo mbele ya vita Bwana anihitaji. Akiniita, kwa upole Nipite njia mpya, Nitajibu, Bwana, Mwaminifu: Utakako, nitakwenda.

Nitakwenda utakako, Bwana, Milimani hata ng’ambo; Nitasema utakacho, Bwana; Nitakuwa utakavyo.

2. Labda leo kuna maneno Natakiwa niseme; Labda kwenye njia za dhambi Yupo asumbukaye. Mwokozi wangu, niongoze, Njiani penye giza, Ili nitangaze neno tamu; Utakacho, nitasema.

Nitakwenda utakako, Bwana, Milimani hata ng’ambo; Nitasema utakacho, Bwana; Nitakuwa utakavyo.

3. Kuna mahali duni hasa Huko kwa walimwengu Pa kwenda kufanyia kazi Kwa ajili ya Yesu. Hivyo najikabidhi kwako, Nikijua napendwa, Hili nafanya kwa moyo wote: Utakavyo, nitakuwa.

Nitakwenda utakako, Bwana, Milimani hata ng’ambo; Nitasema utakacho, Bwana; Nitakuwa utakavyo.