1. Neno huleta amani Kwao washirika. Na mwangaza wa injili Watuelekeza.
2. Maagizo ni ya Mungu Anayetujali. Upendowe mng’aavu Kwao wafuasi.
3. Uongo humong’onyoka, Nazo mila ovu. Wingu lililotishia, Lakiri u Mungu.
4. Heri tujualo Jina, Tuziache dhambi. Roho ataendelea Kutuweka safi.
5. Punde shetani ashindwa Na kuisha dhambi, Shida hazitasumbua, Wala kutuudhi.
6. Tulivyovipata nusu Vitakamilika, Kwani Bwana Mungu wetu Atavirejesha.
7. Kwa subira twaziponya Nafsi hadi aje. Tuzidi kutumikia, Ukombozi uje.