Book cover

Sifa kwa Aliyenena na Bwana

Nyimbo za Dini, 17


0:00 0:00
Introduction
All Verses

1. Sifa kwa aliyenena na Bwana! Nabii huyo alitawazwa. Alifungua kipindi cha mwisho, Watamheshimu mataifa.

Shangwe kwa nabii kwenda mbinguni! Waasi sasa, bure wapinga. Akichangamana nao Miungu; Na kifo hakimshindi tena.

2. Atakumbukwa kwa kufia dini; Jina lake litaheshimiwa! Damu waliyoimwaga waovu, Kwake Mungu itamtetea.

Shangwe kwa nabii kwenda mbinguni! Waasi sasa, bure wapinga. Akichangamana nao Miungu; Na kifo hakimshindi tena.

3. Hauna mwisho ukuhani wake. Milele funguo amiliki. Ataingia katika ufalme, Kutuzwa kati ya manabii.

Shangwe kwa nabii kwenda mbinguni! Waasi sasa, bure wapinga. Akichangamana nao Miungu; Na kifo hakimshindi tena.

4. Dhabihu yatuletea baraka. Kote maovu yatajutiwa. Zindukeni tupiganie haki. Jina la Joseph litakumbukwa.

Shangwe kwa nabii kwenda mbinguni! Waasi sasa, bure wapinga. Akichangamana nao Miungu; Na kifo hakimshindi tena.