1. Sifa kwa Bwana, Mwenyezi, Mfalme wa mbingu! O! Nafsi msifu aliye wokovu wangu! Jumuika Kwa zeze na kinanda, Imbeni kwa kumwabudu!
2. Sifa kwa Bwana! Atawala kwa utukufu. Kwenye mabawa huchukua Watakatifu. Hujaona Mahitaji kakupa Alichokiweka wakfu?
3. Sifa kwa Bwana, mlinzi akuwezeshaye. Hakika fadhila yake daima i nawe. Tafakari Uwezo wa Mwenyezi, Rafiki akupendaye.
4. Sifa kwa Bwana! O! Nafsi yangu umwabudu! Wote ungana na Abrahamu kumwabudu! Na “amina!” Zijumlishe sifa, Sasa tunapoabudu.