1. Mungu wa baba zetu wa kale, Mkonowe watawala kote, Twaimba nyimbo za shukurani Mbele ya Kiti chako cha Enzi.
2. Upendowe ulituongoza; Nchi hii huru umetupa. Kuwa Mlinzi, Mlezi wetu, Njia zako ziwe njia zetu.
3. Vitisho vya vita na taabu, Mkono wako utunusuru. Dini yako safi itujae. Wema wako uturutubishe.