1. Niangaze kwenye giza hili. Niongoze! Ni usiku, na nyumbani mbali; Niongoze! Nioneshe njia ya kupita Hata hatua moja yatosha.
2. Sikuwa hivi, na sikuomba Niongozwe. Nilipenda njia zangu; sasa, Niongoze! Nilipenda raha, bila hofu, Nisamehe kwa kiburi changu.
3. Umenibariki na hakika Upo nami— Kwenye mito, mabonde, milima, Na mauti. Na kukicha nitatabasamu, Na wapendwa, wale wafu wangu!