1. Bwana, dhoruba yavuma! Mawimbi ni makali! Na giza limetanda mbingu. Hifadhi ipo mbali. Hujali twaangamia? Walalaje foo, Hali kila dakika yatisha Na tishio la kifo?
Upepo, mawimbi yaitika: Nyamaza. Ghadhabu ya tufani, iwe Pepo chafu, watu au chochote, Hakuna maji ya kumdhuru Bwana wa bahari, nchi, mbingu. Vyote vitakuitikia: Nyamaza, tulia. Vyote vitakuitikia: Tulizana.
2. Bwana, kwa majonzi mengi Leo nanyenyekea. Moyo umejaa taabu. Niokoe, naomba! Mabubujiko ya dhambi Yalemea roho, Nafa maji! Nazama! Ee Bwana. Ninyoshee mkono!
Upepo, mawimbi yaitika: Nyamaza. Ghadhabu ya tufani, iwe Pepo chafu, watu au chochote, Hakuna maji ya kumdhuru Bwana wa bahari, nchi, mbingu. Vyote vitakuitikia: Nyamaza, tulia. Vyote vitakuitikia: Tulizana.
3. Bwana, vitisho vyakoma. Hali sasa tulivu. Jua la akisi ziwani, Moyoni sina hofu. Kawia, Bwana mpendwa! Nitoe upweke, Nifikie bandari ya kheri Pwani nipumzike.
Upepo, mawimbi yaitika: Nyamaza. Ghadhabu ya tufani, iwe Pepo chafu, watu au chochote, Hakuna maji ya kumdhuru Bwana wa bahari, nchi, mbingu. Vyote vitakuitikia: Nyamaza, tulia. Vyote vitakuitikia: Tulizana.