Book cover

Yesu Ninapokuwaza

Nyimbo za Dini, 73


0:00 0:00
Introduction
All Verses

1. Yesu ninapokuwaza Nafurahi mno; Na nitafurahi hasa Nikikaa kwako.

2. Hakuna cha kukumbuka, Wala jina tamu, Jema na lenye baraka, Kama lako Yesu!

3. Kwa wote wanyenyekevu, Huwapa furaha, Mkarimu kwa waovu Wakikurudia!

4. Yesu, u furaha yetu, U zawadi pia, Ndiwe utukufu wetu, Sasa na daima.