1. Bwana tunakuomba, Bariki mafundisho Na kwa kila mmoja Yabaki mpaka mwisho.
2. Wakati wa ujana, Tutafuata amri. Utuongoze vyema, Tupe nguvu tutii.
3. Baba mwenye huruma, Tutafutapo haki, Utujaze furaha Tunapofanya kazi.
4. Tusamehe makosa; Epusha vishawishi. Ndipo tuishi vyema Kitukufu mbinguni.