Book cover

Iwe Upendavyo, Baba

Nyimbo za Dini, 102


0:00 0:00
Introduction
All Verses

1. Alipokuwa mbinguni Bwana aliteuliwa Kuokoa wenye dhambi; “Iwe upendavyo, Baba.”

2. Mtawala na Mfalme Mnyenyekevu akawa, Wakati na hali zote; “Iwe upendavyo, Baba.”

3. Si miiba, si kejeli Kristo zingemzuia. Hakujali yake nafsi; “Iwe upendavyo, Baba.”

4. Mkate nacho kikombe, Ni kumbukumbu ya Bwana. Tuombe nguvu tuseme, “Iwe upendavyo, Baba.”