Book cover

Mwokozi Amefufuka

Nyimbo za Dini, 112


0:00 0:00
Introduction
All Verses

1. Mwokozi amefufuka, Haleluya! Tuseme na malaika, Haleluya! Ushindi kwake juu, Haleluya! Imba dunia na mbingu, Haleluya!

2. Ukombozi ameleta, Haleluya! Na vita amevishinda, Haleluya! Yesu hana mateso, Haleluya! Na giza tena haliko, Haleluya!

3. Kristo tena anaishi, Haleluya! Nguvu ya kifo i wapi? Haleluya! Afa kutuokoa, Haleluya! Kaburi u wapi sasa? Haleluya!