1. Nilisikia kengele, Zikilia pande zote, Nyimbo zao za upendo: “Amani kwa watu wote.”
2. Niliwazia kengele Zililia siku ile Nyimbo nzuri za Krismasi: “Amani kwa watu wote.”
3. Nilihisi kufa moyo, Amani kutokuwepo, Dunia inakejeli: “Amani kwa watu wote.”
4. Nyimbo zikanikumbusha: Mungu yupo, hajalala, Haki itatushindia, “Amani kwa watu wote.”
5. Nyimbo ziliendelea, Usiku hadi mchana, Kwa sauti ya ahadi: “Amani kwa watu wote.”