Book cover

Bwana, Kwako Naja

Nyimbo za Dini, 125


0:00 0:00
Introduction
All Verses

1. Ninakupenda, Mwokozi, Napita njia yako. Nitainua wengine, Nipate nguvu kwako. Ninakupenda, Mwokozi— Bwana, kwako naja.

2. Mimi nani kuhukumu? Nami siko kamili. Mioyo kimya huficha Masononeko mengi. Mimi nani kuhukumu? Bwana, kwako naja.

3. Nitawajali wengine, Nijifunze kuponya. Wahitaji na wanyonge, Nitawahurumia. Nitawajali wengine— Bwana, kwako naja.

4. Nitapenda ndugu zangu Jinsi unipendavyo. Uwezo wako nipate Nifanye kazi yako. Nitapenda ndugu zangu— Bwana, kwako naja.