1. Wapendwa wa Mchungaji, Ni kondoo wapendwa; Tunu pendo awapalo, Tunu kuliko fedha. Wapendwa wa Mchungaji, Na kondoo “wengine”; Milimani awasaka, Hata kina chochote.
Jangwani watangatanga, Wasumbuka wapweke; Aenda kuwakomboa, Zizini warudishwe.
2. Wapendwa wa Mchungaji, Ndio wanakondoo; Kuna wanaopotea, Wadhoofika huko. Ona, Mchungaji Mwema, Asaka wapotevu, Awarudisha kwa shangwe, Na kwa gharama kuu.
Jangwani watangatanga, Wasumbuka wapweke; Aenda kuwakomboa, Zizini warudishwe.
3. Wapendwa wa Mchungaji, Ni “tisini na tisa.” Apenda wapoteao, Tumaini wakosa. Sikia! Wito wa moyo, Kwa upole asihi: “Hutafuti mpotevu, Aliye mbali nami.”
Jangwani watangatanga, Wasumbuka wapweke; Aenda kuwakomboa, Zizini warudishwe.
4. Malisho yanavutia; Maji yenye uhai. Bwana, kwa ari twajibu, “Ndiyo, tunakubali! Tufanye wachunga wako; Tupe pendo la kina. Tutume mbali jangwani, Kondoo kuwasaka.”
Jangwani watangatanga, Wasumbuka wapweke; Twendeni kuwakomboa, Zizini warudishwe.