Book cover

Kuna Lolote Jema Nimefanya?

Nyimbo za Dini, 128


0:00 0:00
Introduction
All Verses

1. Kuna lolote jema nimefanya? Kuna niliyemuinua? Kuna mwenye dhiki niliyefariji? La sivyo, nimekosa. Niliondolea mtu vikwazo Kwa kujitolea kwangu? Walipata nusuri wachovu nao? Walipoita, nilijibu?

Amka, fanya zaidi Ya kuota u mbinguni. Tenda jema daima, utafurahia Baraka za maadili.

2. Fursa za kazi zipo hata sasa, Nafasi zatujia tele. Chunga usipitwe, usihairishe, Bali nenda kafanye. Ni uadilifu mtu kutoa; Upendo unathawabu. Mtenda jema, yeye ni msaada. Wema sio bure kwa Mungu.

Amka, fanya zaidi Ya kuota u mbinguni. Tenda jema daima, utafurahia Baraka za maadili.