Book cover

Nitakwenda Utakako

Nyimbo za Dini, 154


0:00 0:00
Introduction
All Verses

1. Labda siyo kwenye milima Wala penye tufani, Labda siyo mbele ya vita Bwana anihitaji. Akiniita, kwa upole Nipite njia mpya, Nitajibu, Bwana, Mwaminifu: Utakako, nitakwenda.

Nitakwenda utakako, Bwana, Milimani hata ng’ambo; Nitasema utakacho, Bwana; Nitakuwa utakavyo.

2. Labda leo kuna maneno Natakiwa niseme; Labda kwenye njia za dhambi Yupo asumbukaye. Mwokozi wangu, niongoze, Njiani penye giza, Ili nitangaze neno tamu; Utakacho, nitasema.

Nitakwenda utakako, Bwana, Milimani hata ng’ambo; Nitasema utakacho, Bwana; Nitakuwa utakavyo.

3. Kuna mahali duni hasa Huko kwa walimwengu Pa kwenda kufanyia kazi Kwa ajili ya Yesu. Hivyo najikabidhi kwako, Nikijua napendwa, Hili nafanya kwa moyo wote: Utakavyo, nitakuwa.

Nitakwenda utakako, Bwana, Milimani hata ng’ambo; Nitasema utakacho, Bwana; Nitakuwa utakavyo.