Book cover

Fimbo Ya Chuma

Nyimbo za Dini, 158


0:00 0:00
Introduction
All Verses

1. Kwa Nefi, mwonaji yule, Mungu kafunua, Mfano wa neno lake Ni fimbo ya chuma.

Ishike fimbo ya chuma; Aminifu kweli. Hii fimbo— neno la Bwana— Mwongozo thabiti.

2. Tupo bado safarini, Kwenye majaribu; Tutapitia gizani, Penye hatari tu.

Ishike fimbo ya chuma; Aminifu kweli. Hii fimbo— neno la Bwana— Mwongozo thabiti.

3. Adui akisogea, Kutisha njiani, Tushike fimbo ya chuma, Tuombe auni.

Ishike fimbo ya chuma; Aminifu kweli. Hii fimbo— neno la Bwana— Mwongozo thabiti.

4. Hatua na kwa hatua, Siku hadi siku, Kwa sala na wimbo pia, Tusonge mbele tu.

Ishike fimbo ya chuma; Aminifu kweli. Hii fimbo— neno la Bwana— Mwongozo thabiti.

5. Pumziko li karibu, Yaongoza fimbo, Tutapata utukufu Tukishika neno.

Ishike fimbo ya chuma; Aminifu kweli. Hii fimbo— neno la Bwana— Mwongozo thabiti.