1. Maisha yaliyo mema Huakisi wako wema; Unatubariki, Mungu, Kupitia ndugu zetu.
2. Ni zawadi gani kubwa, Ni zawadi gani bora, Kama walio na Yesu Kukuza imani zetu.
3. Na rafiki kama huyu, Mioyoni atadumu Kutukumbusha vizuri Kukaribia mbinguni.
4. Twakushukuru Mwokozi Kwa marafiki wazuri, Walio waaminifu, Na wanaokuabudu.