Book cover

Dada wa Sayuni

Nyimbo za Dini, 169


0:00 0:00
Introduction
All Verses

1. Dada wa Sayuni, tushirikiane Baraka za Mungu kuzitafuta. Kwa nguvu tuujenge ufalme wake, Kwa wale wanyonge tuwe faraja.

2. Tumepewa ujumbe wa malaika, Na twajivunia kipawa hiki: Tufanye vyote vya utu kwa pamoja Kwa jina la huruma tubariki.

3. Azima na wito wetu ni mpana, Kazi za kiroho tutekeleze. Ni Roho tu atakayetufundisha Tupate hekima tufanikiwe.