Nyimbo Za Dini Pamoja Na Nyimbo Za Watot (1983),
p. 26
Asubuhi Njema
Asubuhi Njema
1. Asubuhi ile njema!
Jua likachomoza.
Na sauti zao ndege,
Zote zilisikika.
Hapo katika kisitu
Joseph kamwomba Baba,
Hapo katika kisitu
Joseph kamwomba Baba.
2. Alipopiga magoti—
Sala yake ya kwanza—
Nguvu za Shetani nazo
Zikamshambulia;
Hakusita kuamini
Mungu atamlinda,
Hakusita kuamini
Mungu atamlinda.
3. Ghafla mwanga ukashuka
Unaozidi jua,
Na mwale wa utukufu
Ukammulikia,
Ndipo wakaja wawili,
Mungu Baba na Mwana,
Ndipo wakaja wawili,
Mungu Baba na Mwana.
4. “Huyu, Mwanangu Mpendwa;
Utamsikiliza!”
Kajibiwa sala yake,
Akamtii Bwana.
Ni furaha iliyoje,
Kumwona Mungu Baba,
Ni furaha iliyoje,
Kumwona Mungu Baba.
Maandishi: George Manwaring, 1854–1889
Muziki: Sylvanus Billings Pond, 1792–1871; umefanyiwa marekebisho na A. C. Smyth, 1840–1909
Maandishi: George Manwaring, 1854–1889
Muziki: Sylvanus Billings Pond, 1792–1871; umefanyiwa marekebisho na A. C. Smyth, 1840–1909