Nyimbo Za Dini Pamoja Na Nyimbo Za Watot (1983),
p. 40
Ewe Baba Yangu
Ewe Baba Yangu
1. Baba yangu, uishiye
Palipo patukufu,
Lini nitarudi kwako,
Na tena nisujudu?
Je, kwako patakatifu,
Niliishi kiroho?
Asili yangu ya kwanza,
Nililelewa kwako?
2. Kwa kusudi la pekee
Naishi duniani,
Na bila ya kumbukumbu
Ya wangu uasili;
Kuna muda nasikia
Nong’ono, “Sio kwenu,”
Na nahisi natokea
Mahali patukufu.
3. Kupitia Roho wako,
Nilikuita Baba.
Hadi kurejeshwa nuru
Sababu sikujua.
Mbinguni kuna Baba tu?
Maana haileti!
Kweli ni mantiki; kweli
Nina mama mbinguni.
4. Niiachapo dunia,
Mwili niulazapo,
Baba, Mama, mtaacha
Niwaone mliko?
Basi nikishamaliza
Kufanya kazi zote,
Ikiwa mtakubali,
Ruhusu kwenu nije.
Maandishi: Eliza R. Snow, 1804–1887
Muziki: James McGranahan, 1840–1907
Maandishi: Eliza R. Snow, 1804–1887
Muziki: James McGranahan, 1840–1907