Nyimbo Za Dini Pamoja Na Nyimbo Za Watot (1983),
p. 52
Sifa Kwake Yeye
Sifa Kwake Yeye
1. Sifa kwa aliyenena na Bwana!
Nabii huyo alitawazwa.
Alifungua kipindi cha mwisho,
Watamheshimu mataifa.
Shangwe kwa nabii kwenda mbinguni!
Waasi sasa, bure wapinga.
Akichangamana nao Miungu;
Na kifo hakimshindi tena.
2. Atakumbukwa kwa kufia dini;
Jina lake litaheshimiwa!
Damu waliyoimwaga waovu,
Kwake Mungu itamtetea.
Shangwe kwa nabii kwenda mbinguni!
Waasi sasa, bure wapinga.
Akichangamana nao Miungu;
Na kifo hakimshindi tena.
3. Hauna mwisho ukuhani wake.
Milele funguo amiliki.
Ataingia katika ufalme,
Kutuzwa kati ya manabii.
Shangwe kwa nabii kwenda mbinguni!
Waasi sasa, bure wapinga.
Akichangamana nao Miungu;
Na kifo hakimshindi tena.
4. Dhabihu yatuletea baraka.
Kote maovu yatajutiwa.
Zindukeni tupiganie haki.
Jina la Joseph litakumbukwa.
Shangwe kwa nabii kwenda mbinguni!
Waasi sasa, bure wapinga.
Akichangamana nao Miungu;
Na kifo hakimshindi tena.
Maandishi: William W. Phelps, 1792–1872
Muziki: Wimbo wenye asili ya Uskoti
Maandishi: William W. Phelps, 1792–1872
Muziki: Wimbo wenye asili ya Uskoti