1. Tumsifu Mungu wetu Aliye mbinguni, Atawala kwa dhamira, Mbingu nazo nchi.
Jina lake liinue; Sifu utawala! Msujudu Bwana Mungu, Mfalme daima.
2. Chini yake, kwa amriye, Sayari na mbingu Huonyesha kila saa Hekima ya Mungu.
Jina lake liinue; Sifu utawala! Msujudu Bwana Mungu, Mfalme daima.
3. Ua dogo liishilo, Ndege wa msimu, Nao pia wanatunzwa; Kawaumba Mungu.
Jina lake liinue; Sifu utawala! Msujudu Bwana Mungu, Mfalme daima.
4. Sauti za kuvutia Nyimbo zimwimbie; Tumsifu, sala zetu Azijibu zote.
Jina lake liinue; Sifu utawala! Msujudu Bwana Mungu, Mfalme daima.