Book cover

Baki Nami; Kumekuchwa

Nyimbo za Dini, 88


0:00 0:00
Introduction
All Verses

1. Baki nami; kumekuchwa. Muda ni jioni; Giza sasa laingia; Haliepukiki. Moyoni mwangu, mwalikwa, Kaa nami kwangu.

Mwokozi baki na mimi; Ona, kumekuchwa. Mwokozi baki na mimi; Ona, kumekuchwa.

2. Baki nami; kumekuchwa. Kuwapo pamoja Kumegusa moyo wangu, Tulipoongea. Umejaza nafsi yangu Kwa kuwa karibu.

Mwokozi baki na mimi; Ona, kumekuchwa. Mwokozi baki na mimi; Ona, kumekuchwa.

3. Baki nami; kumekuchwa. Usiku mpweke Kama hutanena nami, Uniangazie. Giza, linanitishia, Kuingia kwangu.

Mwokozi baki na mimi; Ona, kumekuchwa. Mwokozi baki na mimi; Ona, kumekuchwa.