1. Wimbi la maisha likutosapo,
    Unakata tamaa ushindwapo,
    Hesabu baraka, kwa mojamoja,
    Wema wa Mungu utakushangaza.
  
  
    Zihesabu;
    Kwa mojamoja.
    Zihesabu;
    Ona ya Bwana.
    Zihesabu;
    Kwa mojamoja.
    Hesabu baraka;
    Ona ya Bwana.
  
 
  
    2. Je, unaelemewa na mzigo?
    Msalaba wakushinda uzito?
    Hesabu baraka; shaka ziishe,
    Na kisha utaimba siku zote.
  
  
    Zihesabu;
    Kwa mojamoja.
    Zihesabu;
    Ona ya Bwana.
    Zihesabu;
    Kwa mojamoja.
    Hesabu baraka;
    Ona ya Bwana.
  
 
  
    3. Uwaonapo wengine na mali,
    Kumbuka ahadi zake Mwokozi.
    Hesabu baraka; wingi wa pesa
    Haununui ufalme wa Bwana.
  
  
    Zihesabu;
    Kwa mojamoja.
    Zihesabu;
    Ona ya Bwana.
    Zihesabu;
    Kwa mojamoja.
    Hesabu baraka;
    Ona ya Bwana.
  
 
  
    4. Hivyo matatizo yakukumbapo,
    Mungu yupo nawe, usife moyo.
    Hesabu baraka; na utajaliwa
    Malaika watakusaidia.
  
  
    Zihesabu;
    Kwa mojamoja.
    Zihesabu;
    Ona ya Bwana.
    Zihesabu;
    Kwa mojamoja.
    Hesabu baraka;
    Ona ya Bwana.
  
 
                   
                  
                  
                
                
                
                  Maandishi: Johnson Oatman, Jr., 1856–1922
 Muziki: Edwin O. Excell, 1851–1921