Book cover

Wazee wa Israeli

Nyimbo za Dini, 170


0:00 0:00
Introduction
All Verses

1. Wazee wa Israeli twendeni Popote tuwasake wenye haki, Penye jangwa, bahari na misitu, Tuwalete Sayuni wawe huru.

O! Babiloni, Babiloni twakuaga; Milima ya Efraemu twaenda.

2. Mavuno mengi wavunaji haba; Tukiungana yote twayaweza. Tutenganishe nganona magugu Toka kifungoni wawekwe huru.

O! Babiloni, Babiloni twakuaga; Milima ya Efraemu twaenda.

3. Tuwatembelee nao maskini Wenye njaa na wale wenye dhiki; Tuwafariji kwa injili yake Tuwaonyeshe njia ya milele.

O! Babiloni, Babiloni twakuaga; Milima ya Efraemu twaenda.