1. Japo kuna matatizo,
Jikazeni kwa bidii!
Na siku ya ufufuo
Itaeneza ukweli,
Itaeneza ukweli.
2. Japo shida zatuzonga,
Punde muda si mrefu,
Kristo atakuja tena,
Na wingi wa utukufu,
Na wingi wa utukufu.
3. Msifuni Mungu kwa nyemi;
Furaha yenu idumu.
Japo bado kuna dhiki,
Amani ipo kwa Yesu,
Amani ipo kwa Yesu.
4. Japo tumedhulumiwa,
Na kuporwa na adui,
Ipo ahadi ya Bwana;
Azma yake haikomi,
Azma yake haikomi.
5. Kazi yasonga kwa kasi
Kwa matukio makuu,
Ufalme wa zama hizi
Utajaza ulimwengu,
Utajaza ulimwengu.
6. Japo mwovu atanuna,
Maneno ya manabii
Yatasimama imara;
Hakuna wa kubatili,
Hakuna wa kubatili.
7. Litukuzwe lake jina,
Atumaye watumishi
Kuambia mataifa
Habari ya ukombozi,
Habari ya ukombozi.
Maandishi: Eliza R. Snow, 1804–1887
Muziki: George Careless, 1839–1932