Nyimbo Za Dini Pamoja Na Nyimbo Za Watot (1983),
p. 13
Kazi Ilivyo Tamu
Kazi Ilivyo Tamu
1. Kazi tamu, Mungu wangu,
Jina lako kulisifu,
Pendo lako kuonyesha,
Ukweli wako kusema.
2. Siku tamu ya Sabato,
Ya dunia niachapo.
Nitaimba kwa uzuri
Kwa kinubi cha Daudi!
3. Moyo wangu utasifu
Kazi yako kushukuru.
Neema yako yang’ara!
Wosia wako, hekima!
4. Ni ushindi ulioje
Kwa jina lako milele,
Kwa furaha nikiona
Uso wako uking’aa!
5. Sitasumbuliwa kamwe
Na dhambi, adui yule,
Maadui watashindwa,
Shetani hatasumbua.
6. Na kisha nitayapata
Yote niliyoyataka,
Nitafanya kila kitu
Milele mbinguni juu.
Maandishi: Isaac Watts, 1674–1748
Muziki: John J. McClellan, 1874–1925
Maandishi: Isaac Watts, 1674–1748
Muziki: John J. McClellan, 1874–1925