Number 147
Tupo Waaminifu wa Imani
Tupo Waaminifu wa Imani
1. Eti! Vijana wasite
Haki kuitetea?
Huku asumbua mwovu,
Tuache kupambana? La!
Tupo waaminifu wa imani
Ya wazazi wetu na ya Nabii;
Na kwa Mungu,
Watiifu,
Daima tu waadilifu.
2. Twajua nguvu za giza
Zinampinga Kristo,
Je, watoto wa ahadi
Hawatashika neno? La!
Tupo waaminifu wa imani
Ya wazazi wetu na ya Nabii;
Na kwa Mungu,
Watiifu,
Daima tu waadilifu.
3. Tutatafuta wokovu;
Ukweli tutashika;
Tutasali tuwe macho
Kwa ari ya ujana. Na’m!
Tupo waaminifu wa imani
Ya wazazi wetu na ya Nabii;
Na kwa Mungu,
Watiifu,
Daima tu waadilifu.
4. Twapania kustahili
Ufalme wake Kristo,
Na waaminifu wote
Waliotii neno. Na’m!
Tupo waaminifu wa imani
Ya wazazi wetu na ya Nabii;
Na kwa Mungu,
Watiifu,
Daima tu waadilifu.
Maandishi na muziki: Evan Stephens, 1854–1930