Nyimbo Za Dini Pamoja Na Nyimbo Za Watot (1983),
p. 32
Fanya Yaliyo Ya Haki
Fanya Yaliyo Ya Haki
1. Tenda mema; imeanza siku,
Mwanga na uhuru vyaingia.
Na malaika waandika juu
Kila tendo, hivyo tenda mema.
Tenda mema; matokeo badaye.
Kwa nguvu uhuru pigania;
Kwa moyo shupavu uendelee.
Mungu yupo, hivyo tenda mema!
2. Tenda mema; zafunguka pingu.
Wafungwa uhuru wamepata.
Kwa imani hawana maumivu.
Ukweli wasonga; tenda mema.
Tenda mema; matokeo badaye.
Kwa nguvu uhuru pigania;
Kwa moyo shupavu uendelee.
Mungu yupo, hivyo tenda mema!
3. Tenda mema; uoga uache.
Songa mbele, lengo waliona.
Nayo machozi yatakwisha punde.
Kuna baraka kutenda mema.
Tenda mema; matokeo badaye.
Kwa nguvu uhuru pigania;
Kwa moyo shupavu uendelee.
Mungu yupo, hivyo tenda mema!
Maandishi: Hajulikani, The Psalms of Life, Boston, 1857
Muziki: George Kaillmark, 1781–1835
Maandishi: Hajulikani, The Psalms of Life, Boston, 1857
Muziki: George Kaillmark, 1781–1835